Contribute to the Physical, Mental and Spiritual Development of the Tanzania people through facilitating the Provision of Quality Social Services to all the people regardless of Colour, Race and Creed

Monday, September 16, 2013

Ukerewe Lab Inauguration

Mradi wa ujenzi wa jengo la Maabara katika hospitali ya Wilaya ulianza tarehe  25/12/2012 kwa ufadhili wa watu wa Marekani kupitia taasisi yake ya Centers of Disease Control & Prevention (CDC) chini ya Mkandarasi  SALEM CONSTRUCTION LTD wa Dar es Salaam ikiwa na malengo ya kuboresha miundombinu kwa ajili ya upatikanaji wa huduma bora za maabara katika hospitali sita za wilaya nchini. Hospital nyingine ni Bagamoyo (Pwani), Ludewa (Njombe, Siha (Kilimanjaro), Karume (Kilimanjaro) na Micheweni (Pemba).  Jengo la maabara lilikamilika rasmi mnamo tarehe 25/3/2013 kwa gharama ya dola za kimarekani 550,000 sawa na shillingi za kitanzania 880,000,000.

 
Wilaya ya ukerewe ni kati ya wilaya saba (7) zinazounda mkoa wa Mwanza. Wilaya ina eneo la kilometa za mraba 6400 ambazo nchi kavu ni kilometa za mraba 640 na kilometa za mraba 5760 ni maji ya ziwa Victoria linalotuzunguka. Wilaya inaundwa na Visiwa 38 kati ya hivyo ni Visiwa 15 tu vyenye makazi ya kudumu na 23 ni makazi ya muda kwa wavuvi. Kiutawala wilaya imegawanyika katika Tarafa nne (4), Kata 24 na vijiji 73. Idadi ya wakazi ni 345,147.
Makusudi ya Mradi huu wa ujenzi wa jengo la Maabara ni kupunguza msongamano wa wagonjwa katika jengo dogo la Maabara lililokuwa linatumika hapo awali, ambako lilikuwa na chumba kimoja tu cha kuchukulia vipimo pamoja na kuongeza wigo wa utoaji wa vipimo zaidi na kupelekea kupata huduma bora za afya (Quality health services delivery). Maabara  hii inatumika katika Hospitali ya Wilaya ambayo ni Hospitali ya rufaa kwa vituo 35  katika wilaya  yenye  jumla ya wakazi wapatao 345,147 na ukizingatia  umbali  na ugumu wa usafiri katika Visiwa.
Maabara hii mpya inayo nafasi ya kutosha na jumla ya vyumba ishirini (20) vilivyofuata ramani iliyothibishwa na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii. Maabara pia ina uwezo wa kudumia wagonjwa zaidi ya 160 kwa vipimo mbalimbali kwa wakati mmoja. Aidha vipimo mbalimbali vya VVU na UKIMWI vitafanyika kwa urahisi zaidi kwa vyumba vilivyotengwa, ambapo wilaya ina kiasi cha asilimia 5.1 ya maambukizi na tayari zaidi ya watu 3874 wanaoishi ya virusi vya Ukimwi wapo kwenye huduma za tiba (yaani CTC) wakiwemo watoto 173.
Tofauti na kabla ya jengo hili, vipimo vipya vitakavyopimwa katika maabara hii mpya ni pamoja na;
  • Kupanda na kuotesha vimelea (Culture and Sensitivity)
  •  
  • Kupima vichocheo vya viungo (Enzymes)
  •  
  • Kuhakiki ugonjwa wa kisukari (Glucose Tolerance Test- G.T.T)
  •  
  • Kifua Kikuu kwa kutumia darubini maalum
  •  
  • Kupima Fungasi
  •  
  • Kutenganisha na kutambua aina ya bacteria
  •  
  • Homa ya matumbo (Typhoid)
  •  
  • Vidonda vya tumbo
  •  
  • Magonjwa ya viungo (Rheumatoid factor)
  •  
  • Upimaji wa muda wa kutoka na kuganda kwa damu (bleeding and clotting time)
  •  
  • Kuhakiki kaswende kwa njia maalum ( Treponema Pallidum Hemaglutination Assay – TPHA)
  •  
  • Kuhifadhi sampuli  za vipimo mbalimbali kabla ya kupelekwa kwa Mkemia Mkuu wa serikali (Histopathology)

 
The Lab on outside view
 

This project is funded from the American People in a collaboration with CSSC
 
 
 
 

 

Lab Manager on Reception


 
 
Main Lab

 
Safety Cabinet

 
Refrigerators

 
CD4 Machine

 
Microscope and Biochemistry Machine

 

 
Haemotology Machine

 

 
Safety Cabinet at TB Unit

 
Eye wash Station

 
 
 
 

Fire Extinguisher
 

Ukerewe Lab Staffs on duty
 

Microscope
 

Haematology  Machine at work
 

 

Side view of the Building
 

Front View of the building
 
 
 

CSSC Staffs from left Dr. Msuka, Madina, Dr. Sekule and the last Dr. Suka
 

Waiting for President Kikwete
 

Dr. Mbwambo CSSC Zone Manager on right and Ukerewe Hospital staff
 

Ukerewe Hospital Staffs
 
 
 
 

President Kikwete signing on guest book
 


President Kikwete listening to the CSSC Zone Manager's Speech
 
 

 

 


President Kikwete on Speech
 
 
 

President Kikwete
 


 
 
 

Mr. President Opening up the Lab
 
From Left CSSC Zone Manager Dr. Mwambo, President Kikwete and Ukerewe DMO Dr. Mataka

 

Mr. Emmanuel- CSSC Lab Advisor narrating Mr. President on Lab safety before the tour
 


President on Special Dress (Lab coat)
 

Mr. Pius Msekwa retired Speaker
 
 

The tour is over
 

The President waving to Ukerewe residents
 

President Kikwete and Mr. Ndikilo RC
 

 


No comments:

Post a Comment