Contribute to the Physical, Mental and Spiritual Development of the Tanzania people through facilitating the Provision of Quality Social Services to all the people regardless of Colour, Race and Creed

Wednesday, April 30, 2014

About the simplified life-long antiretroviral treatment (Option B+):

Is the new simplified life-long antiretroviral therapy (Option B+) for all pregnant and breastfeeding women living with HIV. The new treatment is in the form of one pill, taken once a day (compared to the previous treatment of up to six pills per day).This treatment can be provided at the community level, at local primary care facilities. It keeps mothers healthier, as they continue taking it even after giving birth, through breastfeeding and beyond.  CSSC ART program expect  massive expansion of the treatment coverage for both pregnant and breastfeeding women living with HIV. 



Tuesday, April 29, 2014

Inauguration of Option B+: Zero infants HIV infections


PMTCT Clinic



CSSC Regional Coordinator Dr. Bendela, ART Program Manager Dr. Sekule
CSSC Executive Director and Director of Health Services Dr. Balati
welcoming Nyamagana DC: Mr. Baraka Konisaga

Guest of Honor arriving at Sekoutoure ground

Inauguration of the CD4 Facs Calibur Machine at Sekoutoure Hospital
which supported by CSSC 





CSSC PMTCT Officer: Njiimia Mrema welcoming the Guest of Honor to the Counseling room 



CSSC Director of Health: Dr Josephine Balati

CSSC Executive Director Mr. Peter Maduki

CSSC Team: From left Edgar, Lesilwa, Dr. Makongwa, Matafu, Maombi, Dr. Bendela and Kamonga

CSSC Executive Director: Mr. Maduki greet Mwanza RC Eng. Ndikilo

Lega Martin: A woman who is HIV positive testify safe delivery of the kid without HIV infection

Easter Joseph: Testimonies continue

Dr. Msangi

Nyamagana DC: Baraka Konisaka welcoming the Guest of Honor 


Mwanza RC Engineer Ndikilo during the speech 


Mwanza RC Engineer Ndikilo pressing the alarm as a sign of inaugurating Zero infants HIV infection 

Upendo Daima Choir singing  special HIV song

Dr. Mbwambo: CSSC Lake Zone Manager 

RC leaving the Sekoutore Hospital ground 

Uzinduzi wa ZIRO VVU kwa watoto Kanda ya Ziwa

Maandamano ya uzinduzi wa Ziro VVU kwa watoto Mwanza yaliyoanzia viwanja vya Nyamagana hadi Hospitali ya Mkoa ya Sekoutoure











Friday, April 25, 2014

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
UZINDUZI WA KAMPENI MAALUM YA KUTOKOMEZA MAAMBUKIZI YA VIRUSI VYA UKIMWI KUTOKA KWA MAMA MJAMZITO AU ANAYENYONYESHA KWENDA KWA MTOTO (OPTION B PLUS)
HOSPITALI YA MKOA SEKOUTOURE- MWANZA, JUMANNE 29 APRILI, 2014

UTANGULIZI
Tume ya Kikristo ya Huduma za Jamii Tanzania (Christian Social Services Commission – CSSC) ilianzishwa mwaka 1992, kwa ushirikiano kati ya makanisa ya Kiprotestant yaliyoko chini ya Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT) na yale yaliyo chini ya kanisa Katoliki (TEC). Lengo likiwa ni kuwa na chombo maalumu cha kuratibu na kusimamia utoaji wa Huduma bora za afya na elimu kupitia taasisi zilizo chini ya makanisa hayo ili kuongeza ufanisi na ubora wa utoaji Huduma kwa Jamii.
CSSC ni taasisi inayoamini na kufuata sera ya kufanya kazi kwa ubia au mashirikiano (Public Private Partnership - PPP) na serikali katika kuboresha utoaji wa huduma bora ya afya katika Jamii.

MCHANGO WA CSSC KUBORESHA HUDUMA ZA AFYA NCHINI TANZANIA
CSSC ni chombo chenye mchango mkubwa sana katika utoaji wa Huduma za afya na elimu nchini. Wakati CSSC ikichangia 28% ya utoaji Huduma katika sekta ya elimu nchini, kwa upande wa afya, taasisi binafsi zinachangia 36% katika utoaji wa Huduma za afya nchini. Katika ngazi ya halmashauri za wilaya taasisi za makanisa huchangia 62% katika utoaji Huduma za Hospitali na huchangia 56% ya utoaji Huduma hizo za hospitali katika maeneo ya pembezoni zaidi wanakoishi maskini zaidi nchini Tanzania. Kwa upande wa vyuo vya utabibu mchango wa taasisi za makanisa si haba kwani kati ya vyuo vya Manesi 134 vilivyopo nchini, 68 ni vya taasisi binafsi ambapo kati ya hivyo 44 ni vya makanisa. Kati ya vyuo 8 vya madaktari nchini 6 ni vya taasisi binafsi 4 vikiwa vya makanisa. Kati ya wanafunzi 7,458 wa vyuo vya utabibu nchini waliodahiliwa mwaka wa masomo 2011/12, wanafunzi 5,209 walikuwa katika vyuo vya makanisa. Kwa takwimu za mwaka 2008 vyuo vya Manesi vinavyoendeshwa na makanisa vilikuwa vinazalisha 54% ya Manesi wote nchini (MoHSW 2011; CSSC Database 2009 -20013; HSSP III MTR report 2013).

MAPAMBANO YA KUPIGA VITA VIRUSI VYA UKIMWI
Kati ya shughuli zinazofanywa na Taasisi yetu (CSSC),ni kushiriki katika mapambano ya kupiga vita Virusi vya UKIMWI na UKIMWI hapa mkoani Mwanza na nchini kwa ujumla.Tume ya Kikristo ya Huduma za Jamii kupitia mradi wake wa ART inaratibu huduma ya kutokomeza maambukizi  toka kwa mama kwenda kwa mtoto,huduma za tiba kwa watu wanaoishi na virusi vya UKIMWI (WAVIU) katika wilaya zote za mkoa wa Mwanza,wilaya ya Rorya mkoani Mara na mkoa wa Geita ambao tutaanza kuhudumia ifikapo Oktoba Mosi  mwaka huu.

Kampeni ya kutokomeza maambukizi ya virusi vya UKIMWi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto ilizinduliwa na  Rais  wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Jakaya Mrisho Kikwete  mwaka 2012.CSSC kwa kushirikiana na Wizara ya afya inatekeleza mradi huu kwa kutoa huduma za upimaji wa mama wajawazito,wanaonyonyesha  na watoto  waliozaliwa na mama wanaoishi na virusi vya UKIMWI (VVU),utoaji dawa na kutoa elimu kwa jamii juu ya umuhimu wa kujua hali ya maambukizi ya VVU, mkazo pia unatolewa juu ya ushirikishwaji wa wanaume katika suala zima la kuzuia maambukizi ya kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto.
Katika kutekeleza jukumu hilo CSSC kwa kushirikiana na wizara ya Afya inaendelea kutoa ya mafunzo kwa watoa huduma ya afya katika vituo vya kutolea huduma vya mkoa wa Mwanza, ambapo mpaka sasa,watoa huduma wapatao 557 wa kutoka vituo 222 wameshapewa mafunzo ya kutokomeza maambukizi ya VVU kutoka kwa mama kwenda kwa motto Mkoani Mwanza. Hii ni sawa na asilimia 87.4  ya Idadi ya vituo vya afya na watoa huduma  waliotakiwa kupewa mafunzo haya kwa mujibu wa muongozo wa Wizara ya Afya. Kufikia Desemba 2013 jumla ya vituo 149 vilishaanza kutoa huduma ya option B plus. Ambapo jumla ya wamama 704 ( wajawazito 560 na wanaonyonyesha 144) walipatiwa huduma.

UZINDUZI WA OPTION B PLUS MKOANI MWANZA
CSSC kwa kushirikiana na RHMT chini ya uongozi wa mganga mkuu wa mkoa inatarajia kufanya uzinduzi rasmi wa OPTION B Plus mkoani Mwanza tarehe 29/4/2014. Malengo makuu ya uzinduzi huo ni;
  1. Kuhamasisha na kuongeza uelewa kuhusu OPTION B PLUS katika jamii
  2. Kutambua mchango wa watoa huduma wa afya na kuinua ari katika kutekeleza mpango huu
Wakati uzinduzi huu kutakuwa na maandamano (yatakayo anzia katikati ya mji hadi viwanja vya Hospital ya mkoa – Sekou Toure),utoaji wa huduma ya mama na mtoto,shuhuda kutoka kwa wamama wajawazito wanaoishi na VVU ( expert Mothers),hotuba ya mgeni rasmi,risala kutoka kwa wadau mbalimbali  wanaotoa huduma ya kupambana na UKIMWI pamoja na ujumbe wa option B plus kupitia vikundi vya ngoma vya uelimishaji.

HITIMISHO:
Uzinduzi wa OPTION B+ utasaidia wananchi kujua umuhimu wa huduma hii, hivyo wale waliopo katika huduma hiyo, tuna uhakika wataendelea kuitumia na kwa wale ambao hawajaingia katika mpango huu, watahamasika na kuanza kutumia huduma hii. Wito wetu kwenu ninyi waandishi wa habari ni kuwaomba kuhamasisha jamii kuona umuhimu wa huduma hii, ile wale tayari wanamaambukizi wajitokeze sehemu husika kupata huduma. Pia  Kuhamasisha watu wajitokeze kwa wingi katika siku ya uzinduzi rasmi wa huduma hii tarehe 29 April, 2014 katika viwanja vya Hospitali ya mkoa Sekoutoure.
                                                                                        
Ahsanteni sana.
Renatus Sona
Afisa Uhusiano

Tume ya Kikristo ya Huduma za Jamii (CSSC)

TUME YA KIKRISTO YA HUDUMA ZA JAMII TANZANIA CHRISTIAN SOCIAL SERVICES COMMISSION (CSSC) TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
UZINDUZI WA KAMPENI MAALUM YA KUTOKOMEZA MAAMBUKIZI YA VIRUSI VYA UKIMWI KUTOKA KWA MAMA MJAMZITO AU ANAYENYONYESHA KWENDA KWA MTOTO (OPTION B PLUS)
HOSPITALI YA MKOA SEKOUTOURE- MWANZA, JUMANNE 29 APRILI, 2014

UTANGULIZI
Tume ya Kikristo ya Huduma za Jamii Tanzania (Christian Social Services Commission – CSSC) ilianzishwa mwaka 1992, kwa ushirikiano kati ya makanisa ya Kiprotestant yaliyoko chini ya Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT) na yale yaliyo chini ya kanisa Katoliki (TEC). Lengo likiwa ni kuwa na chombo maalumu cha kuratibu na kusimamia utoaji wa Huduma bora za afya na elimu kupitia taasisi zilizo chini ya makanisa hayo ili kuongeza ufanisi na ubora wa utoaji Huduma kwa Jamii.
CSSC ni taasisi inayoamini na kufuata sera ya kufanya kazi kwa ubia au mashirikiano (Public Private Partnership - PPP) na serikali katika kuboresha utoaji wa huduma bora ya afya katika Jamii.

MCHANGO WA CSSC KUBORESHA HUDUMA ZA AFYA NCHINI TANZANIA
CSSC ni chombo chenye mchango mkubwa sana katika utoaji wa Huduma za afya na elimu nchini. Wakati CSSC ikichangia 28% ya utoaji Huduma katika sekta ya elimu nchini, kwa upande wa afya, taasisi binafsi zinachangia 36% katika utoaji wa Huduma za afya nchini. Katika ngazi ya halmashauri za wilaya taasisi za makanisa huchangia 62% katika utoaji Huduma za Hospitali na huchangia 56% ya utoaji Huduma hizo za hospitali katika maeneo ya pembezoni zaidi wanakoishi maskini zaidi nchini Tanzania. Kwa upande wa vyuo vya utabibu mchango wa taasisi za makanisa si haba kwani kati ya vyuo vya Manesi 134 vilivyopo nchini, 68 ni vya taasisi binafsi ambapo kati ya hivyo 44 ni vya makanisa. Kati ya vyuo 8 vya madaktari nchini 6 ni vya taasisi binafsi 4 vikiwa vya makanisa. Kati ya wanafunzi 7,458 wa vyuo vya utabibu nchini waliodahiliwa mwaka wa masomo 2011/12, wanafunzi 5,209 walikuwa katika vyuo vya makanisa. Kwa takwimu za mwaka 2008 vyuo vya Manesi vinavyoendeshwa na makanisa vilikuwa vinazalisha 54% ya Manesi wote nchini (MoHSW 2011; CSSC Database 2009 -20013; HSSP III MTR report 2013).

MAPAMBANO YA KUPIGA VITA VIRUSI VYA UKIMWI
Kati ya shughuli zinazofanywa na Taasisi yetu (CSSC),ni kushiriki katika mapambano ya kupiga vita Virusi vya UKIMWI na UKIMWI hapa mkoani Mwanza na nchini kwa ujumla.Tume ya Kikristo ya Huduma za Jamii kupitia mradi wake wa ART inaratibu huduma ya kutokomeza maambukizi  toka kwa mama kwenda kwa mtoto,huduma za tiba kwa watu wanaoishi na virusi vya UKIMWI (WAVIU) katika wilaya zote za mkoa wa Mwanza,wilaya ya Rorya mkoani Mara na mkoa wa Geita ambao tutaanza kuhudumia ifikapo Oktoba Mosi  mwaka huu.

Kampeni ya kutokomeza maambukizi ya virusi vya UKIMWi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto ilizinduliwa na  Rais  wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Jakaya Mrisho Kikwete  mwaka 2012.CSSC kwa kushirikiana na Wizara ya afya inatekeleza mradi huu kwa kutoa huduma za upimaji wa mama wajawazito,wanaonyonyesha  na watoto  waliozaliwa na mama wanaoishi na virusi vya UKIMWI (VVU),utoaji dawa na kutoa elimu kwa jamii juu ya umuhimu wa kujua hali ya maambukizi ya VVU, mkazo pia unatolewa juu ya ushirikishwaji wa wanaume katika suala zima la kuzuia maambukizi ya kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto.
Katika kutekeleza jukumu hilo CSSC kwa kushirikiana na wizara ya Afya inaendelea kutoa ya mafunzo kwa watoa huduma ya afya katika vituo vya kutolea huduma vya mkoa wa Mwanza, ambapo mpaka sasa,watoa huduma wapatao 557 wa kutoka vituo 222 wameshapewa mafunzo ya kutokomeza maambukizi ya VVU kutoka kwa mama kwenda kwa motto Mkoani Mwanza. Hii ni sawa na asilimia 87.4  ya Idadi ya vituo vya afya na watoa huduma  waliotakiwa kupewa mafunzo haya kwa mujibu wa muongozo wa Wizara ya Afya. Kufikia Desemba 2013 jumla ya vituo 149 vilishaanza kutoa huduma ya option B plus. Ambapo jumla ya wamama 704 ( wajawazito 560 na wanaonyonyesha 144) walipatiwa huduma.

UZINDUZI WA OPTION B PLUS MKOANI MWANZA
CSSC kwa kushirikiana na RHMT chini ya uongozi wa mganga mkuu wa mkoa inatarajia kufanya uzinduzi rasmi wa OPTION B Plus mkoani Mwanza tarehe 29/4/2014. Malengo makuu ya uzinduzi huo ni;
  1. Kuhamasisha na kuongeza uelewa kuhusu OPTION B PLUS katika jamii
  2. Kutambua mchango wa watoa huduma wa afya na kuinua ari katika kutekeleza mpango huu
Wakati uzinduzi huu kutakuwa na maandamano (yatakayo anzia katikati ya mji hadi viwanja vya Hospital ya mkoa – Sekou Toure),utoaji wa huduma ya mama na mtoto,shuhuda kutoka kwa wamama wajawazito wanaoishi na VVU ( expert Mothers),hotuba ya mgeni rasmi,risala kutoka kwa wadau mbalimbali  wanaotoa huduma ya kupambana na UKIMWI pamoja na ujumbe wa option B plus kupitia vikundi vya ngoma vya uelimishaji.

HITIMISHO:
Uzinduzi wa OPTION B+ utasaidia wananchi kujua umuhimu wa huduma hii, hivyo wale waliopo katika huduma hiyo, tuna uhakika wataendelea kuitumia na kwa wale ambao hawajaingia katika mpango huu, watahamasika na kuanza kutumia huduma hii. Wito wetu kwenu ninyi waandishi wa habari ni kuwaomba kuhamasisha jamii kuona umuhimu wa huduma hii, ile wale tayari wanamaambukizi wajitokeze sehemu husika kupata huduma. Pia  Kuhamasisha watu wajitokeze kwa wingi katika siku ya uzinduzi rasmi wa huduma hii tarehe 29 April, 2014 katika viwanja vya Hospitali ya mkoa Sekoutoure.
                                                                                        
Ahsanteni sana.
Renatus Sona
Afisa Uhusiano

Tume ya Kikristo ya Huduma za Jamii (CSSC)